North Eastern Diocese Of The Evangelical Lutheran Church In Tanzania
Siku ya kihistoria katika Dayosisi ya Kaskazini Mashariki
- Details
- Written by Super User
Leo Tarehe 01/12/2019 imekua siku ya kihistoria katika Dayosisi yetu ya Kaskazini Mashariki, Mungu ametupa neema kwa kubarikiwa watheologia 24 kuwa Wachungaji.Ibada iliyo fanyika katika kanisa kuu Lushoto.Ibada imeongozwa na Mhasham Baba Askofu Dr.Stephen Munga wa Dayosisi ya Kaskazini Mashariki akishirikiana na Askofu kutoka Dayosisi ya Lund Sweden, Askofu Johan Tyrberg. Litugia ili ongozwa na msaidizi wa Askofu Mch.Dkt Eberhardt Ngugi .
- Hits: 139
Mahafali ya 30 ya kidato cha nne shule ya sekondari ya Lwandai
- Details
- Written by Super User
Leo tarehe 19 Oktoba 2019 kumefanyika mahafali ya 30 ya kidato cha nne katika shule ya sekondari ya Lwandai inayomilikiwa na Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, ambapo wanafunzi 119 (wa kike 60 na wa kiume 59) wamehitimu. Mgeni rasmi katika mahafali haya alikuwa ni Mhasham Askofu, Dkt Stephen Ismaili Munga aliyewakilishwa na Mkurugenzi wa Huduma za Jamii, Mchungaji Joyce Kibanga. Mahafali haya yalifana sana yakipambwa na vishirikisho mbalimbali toka kwa wahitimu na wanafunzi wengine. Mchungaji Joyce Kibanga aliwaasa wahitimu kuendelea kujitahidi kusoma kwa bidii, na kwamba wazingatie maadili mema katika maisha yao. Mwisho aliwatakia baraka katika mitihani yao inayotazamiwa kuanza Novemba 4 2019. Awali katika hotuba yake, Mkuu wa shule aliwaomba wazazi kuwapeleka watoto wao katika shule hii kujiunga na masomo ya kidato cha tano na sita ambapo vigezo vya kujiunga na kidato cha tano na sita ni ufaulu wa masomo matatu kwa kiwango cha alama C na katika masomo ya mchepuo wa chaguo lake asiwe na F.
- Hits: 644
THE 47TH CLASS VII GRADUATION CEREMONY IRENTE SCHOOL FOR THE BLIND
- Details
- Written by Super User
MAHAFALI YA SHULE YA MSINGI YA WASIOONA IRENTE
Leo Tarehe 20/09/2019 yamefanyika mahafali ya 47 ya darasa la saba tangu kuanzishwa kwa Shule ya Msingi ya Wasioona Irente mwaka 1963. Katika mahafali hayo walihitimu wanafunzi wanane. Mgeni rasmi katika mahafali hayo alikuwa Baba Askofu wa DKMs aliyewakilishwa na Mch Paulo Diu, Mratibu Elimu wa Dayosisi, ambaye aliisihi jamii kutowatenga au kuwadharau watu wenye mahitaji maalumu. Miongoni mwa watu waliohudhuria mahafali hayo ni pamoja na Stephen Shemdoe, Afisa Elimu Maalumu Wilaya ya Lushoto, Glory Mdemu, Afisa Ustawi wa Jamii wa Wilaya ya Lushoto ,Mch Happyness Diu, Mratibu wa Jinsia na Watoto, Wakuu wa vituo vya Irente, shule jirani na wageni mbalimbali. Vilevile kulifanyika harambee ndogo ya kuchangia maendeleo ya shule hii. Awali kabla ya kuingia ukumbini mgeni rasmi alishuhudia maonesho yaliyoandaliwa na walimu na wanafunzi wa shule hii.
- Hits: 123
Blessed day for the Christians of Irente Lutheran parish in Northern Deanery
- Details
- Written by Super User
Tarehe 16/09/2019 in imekuwa siku ya baraka kwa wakristo wa Usharika wa Irente Dinari ya kaskazini, ambapo vijana 41 walipata kipaimara na vijana 3 walibatizwa na kupata kipaimara. Ibada hiyo iliambatana na tukio la ufunguzi wa nyumba ya Mchungaji. Jambo kubwa siku hiyo ni Jubilee ya miaka 27 toka kuanzishwa kwa usharika wa Irente.
Ibada ilingozwa na msaidizi wa Askofu Mch.Dkt Eberhardt Ngugi .
It was a blessed day for the Christians of Irente Lutheran parish in Northern Deanery where by 41 youths confirmed their faith , 3 among them were confirmed and baptized during the Sunday worship service, these celebrations included the 27 years Jubilee of the Irente parish . The worship service was led by the Principal-Dean Rev Dr. Eberhardt Ngugi
The Principal-Dean Rev Dr. Eberhardt Ngugi confirming one of the Confirmands
Mch Dkt Eberhardt Ngugi akibariki vijana wa kipaimara.
Rev James Mwinuka confirming the confirmands
Mch James Mwinuka akitoa mbaraka kwa vijana wa kipaimara
- Hits: 103
Page 1 of 33